USIMDHARAU MTU KWA SABABU YA ALICHONACHO LEO


Emakulata Msafiri

Mwanakwetukids

Kila mtu alimcheka alipobeba kikapu chake kilichokuwa tupu. Hakuna aliyejua kuwa ndani ya kikapu hicho kulikuwa na ndoto kubwa kuliko walivyoweza kufikiria.

Kila asubuhi mtoto mmoja alikuwa akienda sokoni akiwa na kikapu tupu. Watu walimdhihaki wakisema hana kitu cha kuuza.

Baada ya kutoka shuleni alianza kukusanya mbegu za miti ya matunda kutoka nyumbani na kwa majirani. Alizipanda kwenye vifuko vidogo na kuzitunza kwa miezi kadhaa. Siku zilivyopita  miche hiyo ilikua na kuwa mizuri.

Siku moja alirudi sokoni akiwa na kikapu kilichojaa miche ya maembe, mapapai na machungwa. Watu waliinunua yote kwa sababu walitaka kupanda miti kwenye mashamba yao.

Fedha alizopata alizinunulia vitabu vya shule na vifaa vya kujifunzia. Baadaye alianza kupanda miti mingi zaidi.

Wale waliokuwa wakimcheka waligundua kuwa mafanikio huanza na wazo dogo pamoja na uvumilivu.

emakulatemsafiri@gmail.com

0653903872

0/Post a Comment/Comments