Emakulata Msafiri
Mwanakwetukids.com
Maisha yangu yalikuwa ya kawaida sana mwanzoni.
Nilikuwa na marafiki wachache, tulikuwa tunaheshimiana na mambo yalikuwa yanaenda vizuri tu.
Lakini siku moja nilianza kuona kundi fulani la vijana ambao walikuwa tofauti.
Walikuwa wanajiamini sana, wanavaa vizuri na kila mtu alikuwa anawajua. Walionekana kama wanaishi maisha ya “kipekee”.
Ndani yangu nilitamani kuwa kama wao. Nilianza kujikuta nikiwa karibu nao. Mwanzoni walinipokea vizuri. Nilihisi kama nimeingia kwenye level nyingine.
Nilianza kubadilika mavazi, tabia hata jinsi nilivyoongea.
Lakini sikugundua kuwa nilikuwa napoteza mimi halisi. Polepole mambo yakaanza kubadilika.
Walianza kufanya vitu ambavyo sikuvizoea. Mwanzoni nilicheka nikiona kama ni utani.
Lakini kadri siku zilivyopita nilianza kuona hatari yake.
Nilijikuta nafanya mambo ambayo sikuwahi kufikiria kufanya.
Usiku mmoja tukio fulani lilitokea (ambalo sitalisahau). Ndipo niliposhtuka kabisa.
Nilijiuliza: “Haya ndiyo maisha niliyotaka?”
Nilihisi hofu na majuto kwa wakati mmoja. Siku iliyofuata nilifanya uamuzi mgumu kuondoka kwenye lile kundi.
Haikuwa rahisi. Walinicheka, waliniona kama msaliti. Wengine walijaribu kunivuta nirudi.
Lakini nilisimama imara. Nilirudi kwenye maisha yangu ya zamani nikaanza kujijenga upya.
Emakulatemsafiri@gmail.com
0653903872



Post a Comment