Na, Emakulata Msafiri
Kulikuwa na mtoto mmoja aitwaye Juma, aliyekuwa akiishi kijijini na wazazi wake. Juma alikuwa mvivu kupita kiasi. Alikuwa hapendi kwenda shamba, kusoma wala hata kusaidia kazi ndogondogo nyumbani. Wazazi wake walimkanya sana, lakini hakubadilika.
Siku moja, baba yake alimwambia, “Juma, uende shambani ukalime mahindi leo. Ukifanya vizuri, nitakunulia kiatu kipya.” Lakini Juma alipiga miayo na kusema, “Acha tu, nitafanya kesho.”
Juma alianza kujuta, akatambua kuwa uvivu wake ulikuwa umewaumiza hata wazazi wake. Tangu siku hiyo, akaamua kubadilika. Alianza kuamka mapema, kusaidia shambani, na hata kujiunga na darasa la usiku kusoma.
Uvivu huleta hasara, lakini bidii huleta mafanikio makubwa inabidi Kila mmoja ajitume kwa lengo la kuleta mafanikio katika maisha.
emakulatemsafiri@gmail.com
0653903872
Post a Comment